393. Dhambi Ikikulemea
1. Dhambi ikikulemea,
Kwa Bwana rehema;
Hivi sasa tegemea
Neno la salama.
Tegemea, tegemea,
akwita sasa, Ni Mwokozi,
ni Mwokozi, amini sasa.
2. Yesu amemwaga damu,
Ya nyingi baraka;
Nawe sasa oga mumu
Zioshwamo taka.
Tegemea ....
3. Ni njia Yeye hakika,
Huongoza rahani;
Usikawe kumshika,
Uwe barakani
Tegemea ....
4. Karibu nawe wingie
Mwetu safarini,
Twende tukamwamkie,
Milele Mbinguni.
Tegemea ....