405. Mbele Nina Endelea

1.  Mbele ninaendelea, 

    ninazidi kutembea; 

    Maombi uyasikie,

    Ee Bwana, unipandishe. 

          Ee, Bwana, uniinue,   

          kwa imani nisimame;  

          nipande milima yote,   

          Ee Bwana, unipandishe.


2. Sina tamani nikae,

   mahali pa shaka, kamwe; 

   Hapo wengi wanakaa,

   kuendelea naomba. 

          Ee, Bwana....


3.  Nisifungwe na dunia,

    asumbuapo Shetani;

    natazamia mbinguni,

    nitafika na imani. 

          Ee, Bwana....


4.  Nataka nipandishwe juu,

    zaidi yale mawingu; 

    nitaomba nifikishwe,

    Ee, Bwana, unipandishe. 

        Ee, Bwana.... 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya