424. Nionapo Amani Kama Shwari
1. Nionapo amani kama shwari,
Ama nionapo shida;
Kwa mambo yote umenijulisha
Ni salama rohoni mwangu
Salama rohoni,
Ni salama rohoni mwangu
2. Ingawa Shetani atanitesa,
Nitajipa moyo kwani
Kristo ameona unyonge wangu,
Amekufa kwa roho yangu
Salama rohoni …
3. Dhambi zangu zote,
wala si nusu,
Zimewekwa Msalabani;
Wala sichukui laana yake,
Ni salama rohoni mwangu
Salama rohoni …
4. Ee Bwana, himiza siku ya kuja;
Panda litakapolia;
Utakaposhuka sitaogopa;
Ni salama rohoni mwangu.
Salama rohoni…