427. Sioni Haya kwa Bwana
1. Sioni haya kwa Bwana
Kwake nitang’ara!
Mti wake sitakana
Ni Neno imara
Msalaba ndiyo asili
ya mema
Nitatua mzigo hapo;
Nina uzima, furaha daima,
Njoni kafurahini papo
2. Kama kiti chake vivyo,
Ni yake ahadi,
Alivyowekewa navyo,
Kamwe havirudi
Msalaba ndiyo asili …
3. Bwana wangu, tena Mungu,
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu,
Wala kunikana
Msalaba ndiyo asili …
4. Atakiri langu jina
Mbele za Babaye
Anipe pahali tena
Mbinguni nikae
Msalaba ndiyo asili...