436. Yesu Aliniita, "Njoo"

1. Yesu aliniita, “Njoo,

   raha iko kwangu;

   Kichwa chako ukilaze 

   Kifuani mwangu”

   Nilikwenda kwake mara, 

   sana nilichoka;

   Nikapata kwake raha,

   na furaha tena.


2. Yesu aliniita, “Njoo, 

   kwangu kuna maji; 

   Maji ya uzima, bure,

   unywe uwe hai”

   Nilikwenda kwake mara 

   na maji nikanywa: 

   naishi kwake, 

   na kiu kamwe sina tena.


3. Yesu aliniita,” Njoo, 

   dunia ni giza, 

   Ukinitazama nuru takung’arizia”

   Nilikwenda kwake mara

   Yeye jua langu, 

   ni kila wakati mwanga

   safarini mwangu.


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya