436. Yesu Aliniita, "Njoo"
1. Yesu aliniita, “Njoo,
raha iko kwangu;
Kichwa chako ukilaze
Kifuani mwangu”
Nilikwenda kwake mara,
sana nilichoka;
Nikapata kwake raha,
na furaha tena.
2. Yesu aliniita, “Njoo,
kwangu kuna maji;
Maji ya uzima, bure,
unywe uwe hai”
Nilikwenda kwake mara
na maji nikanywa:
naishi kwake,
na kiu kamwe sina tena.
3. Yesu aliniita,” Njoo,
dunia ni giza,
Ukinitazama nuru takung’arizia”
Nilikwenda kwake mara
Yeye jua langu,
ni kila wakati mwanga
safarini mwangu.