420. Ni Salama Mikononi Mwake
1. Ni salama mikononi mwake
Yesu Mwokozi akiwa nami,
Nakingiwa na hatari zote
Katika mkono wake.
:/katika (kiganja cha)
Mkono wake/:
Wala sina hofu siku zote,
Katika mkono wake.
2. Hunishika mikononi mwake,
Nina amani pendoni mwake
Mungu anitoa shaka zote
katika mkono wake
:/katika (kiganja cha)
Mkono wake/:...
3. Anilinda wala haniachi
pendo lake wala halifichi,
Atanipa nguvu siku zote
katika mkono wake
:/katika (kiganja cha)
Mkono wake/:...