343. Mwana wa Mungu Atoka

1.  Mwana wa Mungu atoka

    kwenenda vitani,

    bendera yake nyekundu;

    utamfuata wee; 

    wataka kuungana 

    na maumivu yake?

    Jitwishe msalaba wako,

    nenda nyuma yake.


2.  Stefano aliuawa 

    kwa kumtegemea 

    ndiye aliyemtazama 

    ashindaye kufa. 

    Yeye kama Bwana wake

    wakati wa kufa, 

    akawaombea wale 

    waliomwumiza.


3.  Na wale mitume tena 

    kumi na wawili,

    Roho kawasaidia 

    kwenenda vitani.

    Hawakuogopa kamwe 

    simba wala panga: 

    Roho utusaidie, 

    tukiwafuata.


4.  Jeshi kubwa lasimama 

    waume na wake 

    mbele ya kiti cha Bwana 

    na nguo nyeupe.

    Wakajiponya mbinguni 

    kushinda mashaka.

    Ee Bwana, utubariki, 

    tukiwafuata! 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya