345. Twalima na Kupanda

1.  Twalima na kupanda 

    mbegu shambani tu, 

    kukuza, na kustawisha 

    ni nguvu ya Mungu. 

    Umande hata mvua

    na jua na mwezi, 

    anayetupa haya

    ni Baba Mwenyezi.

    Vitu vyote vyema 

    vyatoka kwake tu, 

    kwa hiyo tumsifuni,

    tumshukuru Mungu!


2.  Vya mbali, vya karibu, 

    vyatoka kwa Mungu, 

    jua, mwezi na nyota,

    kindege, bahari,

    mimea ya mwituni, 

    vyakula vya shamba,

    kwa mchana joto kali, 

    baridi usiku. 

         Vitu vyote …


3.  Ndiye aongozaye 

    mzunguko wa jua, 

    ni chimbuko la mwezi,

    mwendo wa dunia. 

    Huwalisha wanyama, 

    wapate chakula, 

    watoto wetu pia 

    wakae na afya. 

         Vitu vyote … 


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya