347. Walio Watu Wake

1.  Walio watu wake, 

    awajua Bwana. 

    Wakubwa na wadogo 

    nchini popote. 

    Awahifadhi vyema, 

    hawataangamia.

    /: Waishipo, wafapo 

    ni wake daima. :/

 

2.  Ajua kundi lake katika imani. 

    Wategemea yale wasiyoyaona. 

    Wazaliwa kwa Neno, 

    kwa Neno walelewa

    /: nao kanuni yao

     ni Neno la Mungu. :/


3.  Ajua watu wake katika ushujaa

    wa tumaini lao usio mashaka. 

    Ni miti istawiyo

    katika mwanga wake,

    /: mizizi yao hunywa 

    maji ya uzima. :/

 

4.  Ajua watu wake katika upendo 

    uzaao tunda jema 

    lipendezalo mno. 

    Hupenda ndugu zao 

    alivyotupenda, 

    /: na wao hubariki 

     wabarikiwavyo. :/


5. Tusaidie, Bwana, 

   tupate imani, tumaini 

   lidumu, upendo uzidi.

   Na siku zikifika 

   za kukuona Wewe. 

   /: tupate kusimama 

    kuumeni kwako. :/

 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya