348. Kweli Yahuisha

1. Kweli yahuisha, 

   Maneno yenye uzima,

   Muda unatosha, 

   wewe uweze kukoma. 

   Ni faida gani,

   Wapata kwake Shetani? 

   Geukeni kwa Yesu rudini,

   atakuponya dhambini.

       Ee ndugu 

       muda wako unapita. 

       Ya kale yageuka na kupita.

       Yale mapya  

       ndiyo sasa tunapata.


2. Wafikiri nini,  wewe usipofuata 

   mafunzo ya dini, 

   kama  ulivyoyapata?

   Mchana u mwema, 

   usiku unageuka. Shika maonyo

   vema daima, utaona ni baraka. 

        Ee ndugu …


3. Ni huzuni sana,

   kwa watu wengi wa  Mungu,

   kwa kutokazana 

   kuyafuata ya mbingu.

   Wasikia mengi,

   nao wayaacha tena.

   Lakini kwa dhambi zao nyingi

   wanatengwa naye Bwana. 

         Ee ndugu …


4. Ajabu ni wazi, 

   wengi waona aibu,

   Kuifanya kazi ya Bwana

   mwenye thawabu. 

   Wajificha  wengi,

   watenda  kimataifa.

   Wenzangu, ndiyo huzuni nyingi

   ya kuelekea kufa. 

         Ee ndugu ... 


5. Maisha ya wengi, 

   sasa wakata tamaa. 

   Uzito ni mwingi,

   moyoni wajitetea. 

   Waona machozi,

   hao wote wenye dhambi. 

   Kumbuka imemalizwa kazi.

   Yesu ameshinda dhambi. 

         Ee ndugu ...


6. Yesu alifika

   kwa watu kuwakomboa.

   Naye husikika pengi 

   katika dunia.

   Na kila namna ya watu 

   anawatunza. Atoaye 

   wokovu ni Bwana 

   kwa kuwa huwaongoza. 

         Ee ndugu …


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya