350. Maji Yako ya Akiba

1.  Maji yako ya akiba 

    yatakapopungua 

    uwakarimu wenzako

    wasafiri njiani,

    na hayo yatawatosha,

    safari yenu yote.

 

2.  Kapu utakalotoa, 

    litajalizwa tena. 

    Vyakula vikipungua, 

    anga yafunguliwa 

    kilichotosha kwa mmoja,

    kitatosha wawili.


3.  Sadaka iliyo hai, 

    Mungu huibariki. 

    Ghala za dunia hii, 

    nondo watamaliza.

    Utabarikiwa sana 

    hazina ya mbinguni.


4.  Limbikiza juu mbinguni 

    kutu isikofika, 

    sadaka yako iliko 

    ndiko na moyo wako 

    utakapokaa nayo, 

    mbinguni juu milele.


5.  Roho ipendayo ndugu 

    ni maji ya uhai 

    ukimtazama Mwokozi, 

    u tajiri mbinguni, 

    unapopenda wenzako,

    huo ni uhai mpya. 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya