351. Nataka Nimjue Yesu
1. Nataka nimjue Yesu,
na nizidi kumfahamu,
nijue pendo lake, na
wokovu wake kamili.
Zaidi, zaidi,
nimfahamu Yesu,
nijue pendo lake, na
wokovu wake kamili.
2. Nataka nimwone Yesu,
na nizidi kumsikia
anenapo Kitabuni,
kujidhihirisha kwangu.
Zaidi, zaidi …
3. Nataka nifahamu, na
nizidi kupambanua
mapenzi yake, nifanye
yale yanayompendeza.
Zaidi, zaidi …
4. Nataka nikae naye,
kwa mazungumzo zaidi,
nizidi kuwaonyesha
wengine wokovu wake.
Zaidi, zaidi …