353. Twendeni Askari

1.  Twendeni askari, 

    watu wa Mungu; 

    Yesu yuko mbele,

    tumwandame juu; 

    Ametangulia  Bwana vitani,

    twende mbele 

    kwani ndiye amini. 

         Twendeni askari  

         watu wa Mungu: 

         Yesu yuko mbele,

         tumwandame juu.


2.  Jeshi la Shetani, likisikia 

    Jina la Mwokozi litakimbia

    kelele za shangwe zivume nchi;

    Ndugu inueni zenu sauti: 

          Twendeni …


3.  Kweli kundi dogo,

    watu wa Mungu, 

    sisi na mababa tu moja fungu, 

    hatutengwi nao, moja imani, 

    tumaini moja, na moja dini.

           Twendeni...


4.  Haya mbele watu nasi njiani.

    Inueni mioyo nanyi sifuni; 

    Heshima na sifa ni ya Mfalme.

    Juu hata chini, sana zivume.

           Twendeni …


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya