358. Anayemtumaini Mungu

1.  Anayemtumaini Mungu 

    siku zote kwa moyo mkuu, 

    ataona mastaajabu, 

    zikija shida na msiba.

    Anayemngojea Mungu 

    amejenga juu ya mwamba.


2.  Tukisumbuka mchana kutwa

    sababu ya shida zetu:

    Tukilia usiku kucha 

    sababu ya msiba wetu 

    ni bure: Twazidisha tu 

    uchungu wa msiba wetu.


3.  Lakini tukivumilia 

    mizigo tuliyotwikwa,

    na Baba yetu ajuaye 

    vizuri yanayotufaa,

    tutapewa nguvu nyingi 

    za kuchukua huzuni.


4.  Ameiweka saa tayari 

    ya kupunguza mizigo.

    Tukiwa wenye welekevu

    katika kuvumilia, 

    mara atatuokoa

    na kututendea mema.


5.  Katika shida usidhani:

   “Mungu kaniacha sasa:

    Lakini matajiri wote 

    anawapenda vizuri.” 

    Anageuza upesi

    hali ya watu wowote.


6.  Si kazi ngumu kwake Mungu

    kukuza watu maskini, 

    kuwapunguza matajiri 

    wajikuzao wenyewe, 

    Mungu aweza upesi 

    kukuza na kupunguza.


7.  Fuata njia yake Mungu 

    ufanye kazi kwa bidii, 

    umtumaini Mwenye enzi 

    Yeye atakubariki.

    Amtegemeaye Mungu 

    hatakosa msaada wake. 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya