359. Nikiwa na Yesu

1. Nikiwa na Yesu, akiwa nami:

   Mpaka nitakapokufa 

   sisahau pendo lake, 

   sioni huzuni

   naona furaha na amani.


2. Nikiwa na Yesu naacha vyote,

   namfuata Bwana wangu 

   siku zote kwa bidii; sitazifuata

   njia pana za dunia hii.


3. Nikiwa na Yesu nayatumia

   mambo yote ya dunia

   Baba anavyopenda 

   nikimjua Yeye

   siogopi mambo ya dunia.


4. Nilipo na Yesu ndipo pazuri.

   Ninapata mema yote

   kama mrithi wa Mungu;

   ninapewa ndugu wapya ndio

   Wakristo wenzangu.


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya