360. Ninamwambia Mungu
1. Ninamwambia Mungu
aliye Mwenye enzi
mambo yangu yote.
Asiposaidia
kwa tendo na baraka
siwezi kutenda kitu.
2. Nikisumbuka sana,
usiku hata mchana,
ni bure kabisa.
Mungu atamaliza
shughuli zangu zote
kama Yeye apendavyo.
3. Namtumaini Bwana
anayenikingia
hatari na shida.
Nikimfuata Yeye
sitaona hasara,
sitapungukiwa kitu.
4. Ana huruma nyingi
aondoa maovu,
afuta makosa.
Nijapokosa mengi,
hatanitupa mimi,
rehema yake ni kubwa.
5. Nimempa Bwana huyu
moyo na mwili wangu,
hata kufa kwangu.
Akiniita kwake,
nitafuata hima.
Shauri lake ni jema tu.
6. Moyo wangu, tulia!
Umtumaini Bwana
aliyekuumba.
Kumbuka: Baba yako
atakusaidia,
hakosi shauri lolote.