361. Umngojee Bwana

1.  Umngojee Bwana, 

    moyo wangu,

    umwambie yote,

    ana huruma.

    Acha hofu, jua likicha 

    giza linashindwa

    na mchana mzuri. 

    Huzuni zako zikizidi,

    Mungu wa rehema 

    akulinda.


2.  Umngojee Bwana,

    moyo wangu,

    umwambie yote, 

    ana huruma. 

    Zikivuma nguvu za 

    mwovu:

    Bwana anaweza

    kunyamazisha. 

    Wewe mwokozi,

    nakungoja; niokoe nami,

    Mungu wangu!


3.  Umngojee Bwana, 

    moyo wangu, 

    umwambie yote,

    ana huruma.

    Masumbuko yote yaisha 

    na kilio chetu kitageuzwa,

    tutaipata raha bora.

    Tumshukuru Bwana 

    Mungu wetu.


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya