362. Umwekee Mwenyezi
1. Umwekee Mwenyezi
huzuni na shida
ulizo nazo kwako,
ana nguvu zote
Bwana atulizaye
bahari na pepo,
aweza kutuliza
hata moyo wako.
2. Bwana apenda sana
kubariki watu,
wanaokuja kwake
wakimtumaini.
Ukisumbuka sana
kwa uchungu mwingi,
hupati kitu kwake:
Ila ukimwomba.
3. Njia yako ikiwa
na giza na shida;
anazo njia Yeye
za kukuokoa.
Hakuna awezaye
kumzuia Mungu,
akitaka kufanya
mambo yake makuu.
4. Umtegemee Mungu
ukiona shida,
ana rehema nyingi
atakukumbuka,
saa yake ikifika.
Ungoje wakati
wa Bwana, utaona
jua la furaha.
5. Naye akikawia
kukusaidia,
na giza likizidi,
usione shaka:
Ataka kujaribu
tegemeo lako.
Halafu aondoa
shida zako zote.
6. Atafanya vizuri
vyote uombavyo;
Umtegemee Mungu
na kumtumaini.
Mwisho utaingia
mlangoni pa mbingu,
ndipo utamwimbia
nyimbo za kumsifu.