364. Mwanga Mkuu Ujao
1. Mwanga mkuu ujao,
utuangaze!
Tuyapambanue vema
maovu na mambo mema,
/: Utuangaze. :/
2. Tulivyo duniani
hatuna wema,
macho yanaona woga,
mioyo inatetemeka,
/: Hatuna wema. :/
3. Yesu tu ni Mwanga
wenye furaha.
Tupe kuitumaini
enzi ya utengemano,
/: Yenye furaha. :/
4. Mwanga mkuu ujao,
utuangaze!
Roho zetu ziinuke,
na miguu ipate nguvu,
/: Utuangaze! :/