367. Mwokozi Yesu, Utangulie
1. Mwokozi Yesu, utangulie
njia zote za maisha,
nasi tutakufuata,
utuongoze
mpaka mbinguni!
2. Tunapoona shida zozote,
tuzivumilie vema,
tukumbuke; yatupasa
kwenda mbinguni
kwa shida nyingi.
3. Mambo mabaya yakitujia,
tukiona ndugu zetu
wanashikwa na huzuni,
utukumbushe:
Raha i kwako!
4. Utuongoze njiani Yesu;
utulize mioyo yetu
hata siku za huzuni.
Tufungulie
mlango wa mbingu!