370. Baada ya Kazi na Taabu Zote

1.  Baada ya kazi na taabu zote

    nikiingia kwenye furaha, 

    kumwona Yesu,

    kumwabudia,

    kutakuwa furaha yangu kuu. 

         /: Kumwona tu ni furaha.:/ 

          Nikiondolewa shida zote, 

          nikiona uso wa Bwanangu.

 

2.  Mwenye rehema anipendaye

    akinipa kikao mbinguni, 

    nitamfurahia Mponya wangu

    kwa kumwona tu uso kwa uso.

          Kumwona tu … 


3.  Pale mbinguni kwenye furaha

    nitaonana na ndugu wengi.

    Lakini kumwona Bwana Yesu

    kutakuwa furaha kabisa. 

            Kumwona tu … 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya