371. Kwa Furaha ya Mbinguni
1. Kwa furaha ya mbinguni
umeitwa roho yangu, furahi!
Yesu akufungulia mlango wake,
ruka kwake kama tai.
2. Nitakaza mwendo sana
nifikie kundi la wateule,
waimbao na kusifu Bwana
Yesu pamoja na malaika.
3. Yesu Bwana wangu ng’oa
nanga ya mashua yangu upesi,
niingie bandarini mwa amani
na kuona raha kuu.
4. Yesu wangu sitakoma kukusifu,
kwani umeniponya.
Roho yangu yatamani kukuona;
Bwana njoo, nichukue!
5. Unaweza kwa haraka
kugeuza woga uwe furaha.
Unatupitisha kufa kama ndoto:
mara tutafufuka.
6. Umevumilia shida hata kufa
tusishindwe na kifo.
Sasa kufa kumeshindwa,
nao mwili wangu utafufuka.