376. Yasikilizeni Haya

1. Yasikilizeni haya

   watu wa dunia wote: 

   Mwokozi mara ya pili 

   yuaja atuamue.


2. Haji tena kama kwanza

   na hali ya umaskini.

   Ila kwa kuzionyesha 

   nguvu zake duniani.

 

3. Hao wampendao sasa

   weupe hata weusi. 

   Watamwona akishuka 

   na enzi kuu mawinguni.


4. Siku hiyo ya hukumu 

   mimi nitakuwa wapi,

   watakapoitwa wote,

   walalao kaburini?


5. Yesu Bwana nakuomba:

   Sasa unihurumie,

   kuitenda kazi yako,

   hata urudipo hapa!

 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya