377. Atashuka na Mawingu

1. Atashuka na mawingu 

   aliyewambwa mtini,

   na watakatifu wengi 

   watamtukuza sana. 

      /: Haleluya, Haleluya,  

        Haleluya, :/  

        Yesu anatujia! 


2. Kila jicho litamwona 

   katika enzi yake,

   nao waliombeza 

   wataogopa wote, 

       /: Watalia, watalia, 

        watalia, :/  

        wakimwona Mwokozi.


3. Na alama za vidonda

   hata sasa anazo,

   nao watumishi wake 

   wakombolewa nazo, 

       /: alipata, alipata, 

       alipata, :/ 

       makovu kweli kwao.


4. Wapaangukia wote  

   penye kiti cha enzi.

   Vaa Mwokozi nguvu zote 

   Njoo sasa kumiliki! 

     /: Njoo upesi! Njoo upesi!

      Njoo upesi! :/  

      Tunakuomba Bwana. 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya