384. Mungu Akitupa Kipaji
1. Mungu akitupa kipaji
kilicho kizuri zaidi
atusafirisha duniani,
tuone mazuri yake.
2. Mwoga hataki kwenda mbali,
hupenda kuwa kwao tu,
afanana na vifaranga
wasiotoka kwa mama.
3. Mito yaporomoka sana
na ndege wanaimba juu,
tunashirikiana nao
kwa furaha za mioyo.
4. Mungu wetu na asifiwe!
Hulisha ndege, wanyama,
dunia na mbingu ni zake,
yee hatatusahau nasi.