385. Nitayainua Macho Yangu
Nitayainua macho yangu
niitazame milima.
Msaada wangu utatoka wapi?
Msaada wangu u katika Bwana.
Aliyezifanya mbingu na nchi.
Asiuache mguu wako usogezwe.
Asisinzie akulindaye.
Naam, naam, naam.
Hatasinzia wala hatalala usingizi.
Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
Bwana ndiye mlinzi wako.
Bwana ni uvuli
mkono wako wa kuume.
Jua halitakupiga mchana
wala mwezi wakati wa usiku.
Bwana atakulinda
na mabaya yote.
Bwana atakulinda
na mabaya yote.
Atakulinda nafsi yako.
Bwana atakulinda,
Utokapo na uingiapo.
Tangu sasa na hata milele