386. Aitwa na Simanzi
1. Aitwa wa simanzi
Mwana wa mwenye enzi,
Mwenye mengi mapenzi,
Haleluya Bwana Yesu.
2. Alikuwa dhikini,
Bwana Mwokozi wangu
Akatoka mbinguni,
Haleluya Bwana Yesu.
3. Tu wenye dhambi sana,
Kwake dhambi hakuna,
Na Mungu twapatana
Haleluya Bwana Yesu
4. Akapata uchungu
Akalia dhikini
Sasa yuko mbinguni
Haleluya Bwana Yesu
5. Punde atarejea
Yesu kutunyakua
Ndipo tutamwimbia
Haleluya Bwana Yesu