390. Bwana Asema Nimtume Nani

1. Bwana asema 

   Nimtume nani

   /:Na ni nani  

   atakayekwenda 

   badala yetu:/ 

       Nitume mimi Bwana 

       X 4 X 2


2. Midomo yangu

   Michafu sana

   /:Uichome kwa kaa 

   la moto unitakase:/  

        Nitume mimi....


3. Ninaogopa

   Umri  mdogo

   /:Kuhubiri Neno lako

   Bwana huko niendako:/   

         Nitume mimi....


4. Waniambia:

   “Usiogope, 

   /:utapata ujasiri  

    mwingi: kutoka kwangu.”:/ 

            Nitume mimi.... 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya