391. Bwana Mungu, Nashangaa
1. Bwana Mungu,
nashangaa kabisa
nikitazama kama vilivyo;
nyota, ngurumo,
vitu vingi vyote
viumbwavyo
kwa uwezo wako
/: Roho yangu na ikuimbie
Jinsi wewe ulivyo Mkuu.:/
2. Nikitembea pote duniani,
ndege huimba, nawasikia;
milima hupendeza macho sana,
upepo nao nafurahia
/:Roho yangu…
3. Nikikumbuka kama
Wewe Mungu
ulivyompeleka mwanao,
afe, azichukue dhambi zetu
kuyatambua ni vigumu mno.
/: Roho yangu.....
4. Yesu Mwokozi utakaporudi
kunichukua kwenda
mbinguni, nitashukuru
na kwimba milele
Wote wajue jinsi ulivyo.
/:Roho yangu …