392. Bwana Yesu Aliteswa
1. K: /:Bwana Yesu aliteswa,
W: Bwana, kweli Bwana
walimtenga Bwana:/
/:Wanafunzi walimtesa
Bwana, wakamwacha
peke yake, Bwana.:/
K: /:Kweli Yesu aliteswa,:/
W: /:Bwana, walimtesa
msalabani, Bwana.:/
2. K: /:Na askari wakambeza,
W: Bwana, wakamwudhi
kwa Pilato, Bwana:/
/:Nguo zake wakamvua,
Bwana, wakamvika vazi
safi, Bwana.:/
K: /:Kweli Yesu aliteswa../
3. K: /:Hata taji ya miiba,
W: Bwana, wakamvika
kwa dhihaka, Bwana:/
/:Kwa dharau
wakaweka, Bwana,
mkononi mwake
mwanzi, Bwana.:/
K: /:Kweli Yesu aliteswa../
4. K: /:Katemewa mate Yesu,
W: Bwana, akapigwa
pigwa kichwa, Bwana:/
/:Na mzaha wakafanya,
Bwana, wakimsujudia
Yesu, Bwana.:/
K: /:Kweli Yesu aliteswa.../
5. K: /:Hapo wakamsulibisha,
W: Bwana, wakampiga
misumari, Bwana:/
/:Vazi lake wakataka,
Bwana, wakalipigia
kura, Bwana.:/
K: /:Kweli Yesu aliteswa..../
6. K: /:Na wengine wakasema,
W: Bwana, kwamba Yesu
na ashuke, Bwana:/
/:Walakini kasamehe,
Bwana, wakosaji wake
wote, Bwana.:/
K: /:Kweli Yesu aliteswa.../
7. K: /:Ndugu zangu, tufikiri
W: Vema, dhambi zetu
zimemtesa, Bwana:/
/:Kwa upendo wa ajabu,
Bwana, ametupa
msamaha, Bwana:/
/:Siku zote tumshukuru,
Bwana yote
ametufanyia, Bwana.:/