394. Deni ya Dhambi Ilimalizikia

1. Deni yangu ya dhambi, 

   Yesu amelipa.

   Kwake Msalabani 

   Nilipewa Uzima

        Deni ya dhambi,

        Msalabani 

        Ilimalizikia

        Ni huru kabisa.


2. Bwana Yesu asema,

  “Mwanangu dhaifu,

   Uwezo na ushindi

   Hupatikana kwangu.” 

        Deni ya dhambi,...


3. Bwana, kweli naona, 

   Nguvu zako pekee 

   Huondoa ukoma, 

   Niwe kipya kiumbe. 

        Deni ya dhambi,...


4. Sina wema moyoni, 

   Nidai neema, 

   Nakubali kabisa,

   Kwa damu kusafiwa.

       Deni ya dhambi,...


5. Hata huko Mbinguni,

   Miguuni pake,

   “Yesu alinifia,” 

    Nitaimba milele.

           Deni ya dhambi,...


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya