419. Ni Nguvu Ituongozayo
1. Ni nguvu ituongozayo
wote sasa (milele)
Ni nguvu itokayo juu
Kwa Baba Mungu, ya uzima.
Mimi sina kitu kistahilicho
Ee Mwokozi (ila mimi) mimi,
nitumike, Katika kazi yako
ya uzima ningalipo hai.
2. Utupe vipawa toka kwako
mbinguni (daima)
Ni nguvu itokayo juu
tushukiayo daima.
Tubariki sisi sote
Mwokozi maishani
Mimi (hata mimi)
nitumike katika kazi
yako ya uzima ningalipo hai
3. Tuvike utakatifu
wako Bwana ee (twaomba)
Tuvike uwezo wako
ulio hai, tuhuike.
tubariki sisi sote
Mwokozi maishani.
Sisi (hata sisi) tutumike,
katika kazi yako
ya uzima tungalipo hai.