400. Imezuka Siku ya Neema
1. Imezuka siku ya neema,
mfano wa pambazuko;
yenye mwanga toka
Mungu juu furaha ikamilishwe.
Mungu ndiye nuru gizani
akae mioyoni mwetu
2. Imezuka siku ya neema,
Mwokozi katutokea;
ulimwengu wote upewe
furaha pasipo mwisho.
Yesu atupenda kabisa,
fedheha amefukuza.
3. Alibeba dhambi, si zake,
alipotundikwa mtini.
Kifo hakikumweza Kristo.
Mwamba akauondoa,
Ili sisi na jeshi la juu
tumwimbie siku zote.
4. Baada ya siku hamsini
akatumwagia roho,
ili tusibaki gizani,
na kupotelea mbali.
Moto wake watutakasa,
na kutuponyesha kweli.
5. Safari ya mwisho yaiva,
tuitwapo naye Kristo.
Sote tutaimba kwa shangwe
pamoja na wambinguni.
Tukiishi mwangani mwake,
tukimhimidi milele.