403. Katika Neema ya Yesu

1. Katika neema ya Yesu 

   nimeokolewa, 

   nilipotea dhambini,

   kipofu rohoni.


2. Bali neema ya Yesu 

   yanitosha sana 

   ilinifumbua macho 

   ikanifungua.


3. Nilikuwa mwenye hofu

   nilifungwa nazo,

   nimefunguliwa sasa

   kwa neema ya Yesu.


4. Nitamsifu Bwana wangu

   maishani mwote, 

   kwani nina ushirika

   Msalabani mwake.


5. Tutakapofika wote 

   mbinguni kwa Mungu, 

   tutashukuru neema

   ya Yesu milele.


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya