407. Mibaraka Tupe Mibaraka
1. Mibaraka tupe mibaraka
Mibaraka tupe mibaraka
Toka kwako.
Mungu Baba Mungu twakuomba,
/:Tunakuomba libariki
Kanisa lako Baba:/
Liwe na umoja na upendo.
2. Wachungaji na Maaskofu,
Wachungaji na Maaskofu
wabariki,
Na Wainjilisti wabariki.
/:Uwape moyo wa hekima
katika kazi yako:/
Wajenge Kanisa kwa upendo
3. Mungu Baba Mungu twakuomba
Mungu Baba Mungu twakuomba
tubariki;
Hata na Wakristo wabariki
/:utupe moyo wa hekima katika
kazi yako:/
Tujenge Kanisa kwa upendo.
4. Waamini pote duniani Waamini
pote duniani wabariki;
Hata na Wazee wa Kanisa
/:uwape moyo wa hekima
katika kazi yako:/
Wajenge Kanisa kwa upendo.