409. Mjini Kwake Nazareti

1.  Mjini kwake Nazaret

    kasema Yesu wazi,

    yakuwa kwake unabii

    wa kale umetimia.

        /:Kusaidia maskini,   

         vipofu nao waone, 

         wafungwa wawe huru tu,  

         wasetwa wawe wazima.:/


2.  Wazee walishangazwa tu 

    na mahubiri yake. 

    Huenda huyu ni nabii

    na hata Kristo Masihi.

       /:Kusaidia maskini,...


3.  Maisha’ke shuhuda kuu, 

    maneno yake kweli. 

    mpaka kufa kawa mtii,

    kawambwa msalabani.  

        /:Kusaidia maskini,...


4.  Wenzangu, muwe mashujaa,

    kumshuhudia pote.

    Mwokozi Yesu yu pekee,

    na hivyo akatujia. 

          /:Kusaidia maskini,... 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya