410. Mtolee Bwana

1. Mtolee Bwana  katika maisha 

   matunda ya pendo,

   yale yapasayo, 

   tumtolee Bwana.

   Tushukuru yale yatokayo kwake 

   kwa neema kubwa. 

      /:Tutoe sadaka  

       tumshukuru Bwana:/


2. Atupa maisha, akili, uweza;

   atupa nyakati za kufanya kazi; 

   na hiyo ni neema. 

   Na mali nyingine zinatoka

   kwake kutufurahisha. 

       /:Tusifu na nini 

       kwa vipaji vingi?:/


3. Sisi twazaliwa, katika ukiwa.

   Mungu peke yake, 

   ndiye atoaye; 

   kwetu kwa huruma. 

   Tu wakili wake; 

   hayo tuyatunze na tusitawanye.

       /:Kutoa tutoe;  

        talanta ni zake.:/


4. Fundisho ni kubwa:

   Mjane katoa mali yake yote,

   ya nyumbani mwake; 

   kumshukuru Bwana. 

   Kutoa ni haja; 

   tena ni ibada kwake Yesu Bwana.

         /:Tutoe sadaka; 

          tumshukuru Mola.:/


5. Tunapochunguza tunavyotumia, 

   tutoe mioyo,  tuache uchoyo; 

   kwani atupenda.

   Kwa kila wakati; 

   yeye ni mlinzi, anatuongoza.

        /:Tutoe kwa Bwana; 

        hili linapasa.:/ 


6. Ingawa Mwokozi Yeye ni tajiri 

   aliacha Yeye utajiri wake 

   kututajirisha.

   Alibeba Yeye ufukara wote

   kweli ni neema. 

        /:Kwa pendo katenda 

         kwetu yote mema.:/


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya