412. Mungu Ulisema
1. Mungu ulisema, giza ilikoma;
Twashukuru.
Twakusihi sote, duniani mwote,
na kwa watu wote, iwe nuru.
2. Yesu ulikuja, ulituletea
nuru kuu;
Macho kwa vipofu,
maisha kwa wafu:
nasi twakusifu, twashukuru.
3. Roho kiongozi, Roho wa mapenzi
tia nuru;
mwovu hata sasa
watu huwatosa.
Twakuomba hasa, iwe nuru.
4. Mungu wa Utatu,
mwanga wao watu,
tuwe nuru;
twende kwote, kwote,
wafundishwe wote:
duniani mwote iwe nuru.