414. Mwokozi Umeokoa
1. Mwokozi umeokoa
nimekuwa wako Wewe.
Damu imenisafisha,
Sifa kwa Mwana Kondoo.
Utukufu, Haleluya,
Sifa kwa Mwana Kondoo.
Damu imenisafisha,
utukufu kwa Yesu.
2. Nilijitahidi sana
ila sikupata raha
bali kwa kumtegemea
nilipata baraka.
Utukufu Haleluya…
3. Daima namwegemea
damu ikifanya kazi
Nikioga kwa chemchemi
itokayo Mwokozi.
Utukufu Haleluya…
4. Sasa nimewekwa wakfu
nitaishi kwako Wewe:
Fahari nashuhudia
Ya wokovu wa bure.
Utukufu Haleluya...
5. Nasimama kwake Yesu
ameponya roho yangu,
Ameniondoa dhambi
anifaye mzima.
Utukufu Haleluya…
6. Nilifungwa kifungoni
niliteswa nazo dhambi
Nilifungwa minyororo
Yesu kanifungua
Utukufu Haleluya…
7. Sifa ameninunua!
Sifa, nguvu za wokovu!
Sifa Bwana huhifadhi!
Sifa zake milele
Utukufu Haleluya…