416. Ndiyo Damu ya Baraka
1. Ndiyo damu ya baraka
ituoshayo wakosa,
kwake Bwana twaokoka,
nasi twamsifu sasa.
Nimestahili hukumu,
siwezi kujitakasa
Nioshe katika damu,
Takuwa safi kabisa.
Safi kabisa; safi kabisa!
Nioshe katika damu
Takuwa safi kabisa.
2. Yesu alivikwa miiba
Na kuangikwa Mtini,
Na maumivu si haba
Yaliyompata chini
Nataka kijito hicho
Niende kuoga sasa;
Ndicho kinitakasacho
Nami ni safi kabisa.
Safi kabisa, safi kabisa!
Ndicho kinitakasacho,
Nami ni safi kabisa.
3. Baba, kweli nimekosa,
moyo wangu ni dhaifu;
Dhambi ni nyingi kabisa
Nipate wapi wokovu?
Yesu kijitoni pako
naja naamini sasa
Nioshe kwa damu yako,
Takuwa safi kabisa.
Safi kabisa, safi kabisa!
Nioshe kwa damu yako,
Takuwa safi kabisa.