418. Nimekombolewa na Yesu

1. Nimekombolewa na Yesu

   Aliyenirehemia;

   Kwa bei ya mauti yake

   Nimekuwa mtoto wake 

          Kombolewa!  

          Nakombolewa na damu; 

          Kombolewa! 

          Mimi mwana wake kweli


2. Kukombolewa nafurahi, 

   Kupita lugha kutamka;

   Kulionyesha pendo lake,

   Nimekuwa mtoto wake.

            Kombolewa! …


3. Nitamwona uzuri wake,

   Mfalme wangu wa ajabu; 

   Na sasa najifurahisha katika

   neema yake 

            Kombolewa! …


4. Najua taji imewekwa 

   Mbinguni tayari kwangu; 

   Muda kitambo atakuja

   Ili alipo, niwepo 

            Kombolewa! … 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya