423. Ninamwamini Baba Mungu
1. K: Ninamwamini Baba Mungu,
W: Mwenye enzi yote;
K: Muumba nchi pia mbingu,
W: Vilivyomo vyote;
K: Pia Kristo aaminiwa,
W: Huyo mwana wake;
K: Alikuja kwa kuzaliwa
W: Kubwa pendo lake
K: Imani
W: Ya kanisa moja
K: la Kristo.
W: Kweli amekuja
K: Yu msingi
W: wa watakatifu
K: Ni Bwana,
W: ndiye mtukufu.
2. K: Alichukua msalaba,
W: watu waokoke;
K: Ni upendo wa Mungu Baba,
W: utokao kwake;
K: Aliyapata hayo mazito,
W: Kwa ajili yetu;
K: Zamani hizo za Pilato,
W: Walimtesa watu.
K: Imani ...
3. K: Bwana aliyesulubiwa,
W: kwa dhambi za sisi;
K: upendo kweli ni mkubwa,
W: kwa wote waasi;
K: Na kaburini alizikwa,
W: Kwa yetu maovu;
K: Kuzimuni walishukiwa,
W: Kweli ana nguvu.
K: Imani ...
4. K: Siku ya tatu kafufuka,
W: kamshinda mwovu;
K: Yuko mbinguni hutukuka,
W: kaleta wokovu;
K: Kristo kakaa kuumeni,
W: ni kwa Baba yake;
K: Atajashuka duniani,
W: Kwa viumbe vyake.
K: Imani...
5. K: Wote mwisho
tutakusanywa,
W: tuwe mbele zake;
K: Kila mmoja tuhukumiwa,
W: kwa matendo yake;
K: Ninamwamini Roho pia,
W: Mtakatifu Mungu;
K: Uhuisho hunipatia,
W: Yu Mfariji wangu.
K: Imani...
6. K: Kanisa moja takatifu,
W: Washirika kweli;
K: Ondoleo la upunjufu,
W: kufufuka mwili;
K: Heri mbinguni tutakuwa,
W: na furaha tele;
K: Uzima tutashirikishwa,
W: Ule wa milele.
K: Imani...