423. Ninamwamini Baba Mungu

1. K:  Ninamwamini Baba Mungu,

   W:  Mwenye enzi yote; 

   K:  Muumba nchi pia mbingu, 

   W:  Vilivyomo vyote; 

   K:  Pia Kristo aaminiwa, 

   W:  Huyo mwana wake; 

   K:  Alikuja kwa kuzaliwa 

   W:  Kubwa pendo lake

   K:  Imani

   W:  Ya kanisa moja

   K:  la Kristo. 

   W:  Kweli amekuja

   K:  Yu msingi 

   W:  wa watakatifu

   K:  Ni Bwana, 

   W:  ndiye mtukufu.


2. K:  Alichukua msalaba, 

   W:  watu waokoke;

   K:  Ni upendo wa Mungu Baba,

   W:  utokao kwake; 

   K:  Aliyapata hayo mazito, 

   W:  Kwa ajili yetu;

   K:  Zamani hizo za Pilato, 

   W:  Walimtesa watu. 

   K:  Imani ...


3. K:  Bwana aliyesulubiwa, 

   W:  kwa dhambi za sisi;

   K:  upendo kweli ni mkubwa,

   W:  kwa wote waasi;

   K:  Na kaburini alizikwa,  

   W:  Kwa yetu maovu;

   K:  Kuzimuni walishukiwa,

   W:  Kweli ana nguvu.

   K:  Imani ...


4. K:  Siku ya tatu kafufuka, 

   W:  kamshinda mwovu;

   K:  Yuko mbinguni hutukuka,

   W:  kaleta wokovu;

   K:  Kristo kakaa kuumeni, 

   W:  ni kwa Baba yake;

   K:  Atajashuka duniani, 

   W:  Kwa viumbe vyake.

   K:  Imani...


5. K:  Wote mwisho 

       tutakusanywa,

   W:  tuwe mbele zake; 

   K:  Kila mmoja tuhukumiwa,

   W:  kwa matendo yake; 

   K:   Ninamwamini Roho pia, 

   W:  Mtakatifu Mungu; 

   K:   Uhuisho hunipatia,

   W:  Yu Mfariji wangu.

   K:  Imani...


6. K:  Kanisa moja takatifu,  

   W:  Washirika kweli; 

   K:  Ondoleo la upunjufu,

   W:  kufufuka mwili;

   K:  Heri mbinguni tutakuwa, 

   W:  na furaha tele;

   K:  Uzima tutashirikishwa,

   W:  Ule wa milele.

   K:  Imani... 


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya