425. Shusheni Nyavu Zenu
1. “Shusheni nyavu zenu
Palipo maji mengi
Mtapata mavuno,”
Bwana amesema:
Simoni akasita,
“Mbona tumesumbuka
usiku kucha bure”
:/: Akasema, Nenda!:/:
2. Ee Bwana umesema,
tukawavue watu
vilindini mwa dhambi
za ulimwengu huu.
Simoni akasita,
“Mbona tumesumbuka
Usiku kucha bure;
:/:Nami nitakwenda!”:/:
3. Simoni alipata
baraka za ajabu
aliposhusha nyavu
katika bahari.
Ee Bwana twakuomba
Utujalie nasi,
Tufanye upendavyo:
:/:siku zetu zote:/:
4. Sisi sote Wakristo
tushushe nyavu zetu,
tukawavue watu
waje kwa Mwokozi.
Kwa jina lake Yesu
hatutazipoteza
Baraka toka Mungu:
:/:Sifa zake Bwana!:/: