426. Sifuni Mungu

Sifuni Mungu 

kwa maana yeye

ni mwenye pendo kuu.

Sifuni Mungu kwa 

maana yeye ni mkuu

   

1. Ameturuzuku yeye pekee 

   kwa yanayofaa; kwetu ni nafuu.

   Ameturuzuku yeye pekee 

   kwa yanayofaa:

   ni ya neema tu. 

         Sifuni Mungu...


2. Kamtuma Mwokozi bila mawaa,

   kutoa balaa na hata fadhaa. 

   Kamtuma Mwokozi bila mawaa,

   kutoa balaa ni ya neema tu. 

          Sifuni Mungu...


3. Na tumtumikie kwa kila saa,

   bila kukataa wala kunyamaa. 

   Na tumtumikie kwa kila saa,

   bila kukataa ni ya neema tu. 

          Sifuni Mungu... 

Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya