428. Tangu Siku Hiyo

1.  Tangu siku hiyo aliponijia,

    Akae moyoni mwangu, 

    Sina giza tena ila mwanga pia

    Kwa Yesu Mwokozi wangu. 

        Amani moyoni mwangu, 

        Kwa Yesu, Mwokozi wangu; 

        Sina shaka kamwe  

        kwa sababu Yeye 

        Yu nami moyoni mwangu.


2.  Sina haja tena ya kutangatanga,

    Ndiye kiongozi wangu, 

    Dhambi zangu zote 

    zimeondolewa,

    Na Yesu, mwanawe Mungu. 

          Amani moyoni …


3.  Matumaini yangu ni ya hakika,

    katika Mwokozi wangu. 

    Hofu zangu na hamu 

    zimeondoka

    kwa kuwa ninaye Yesu 

           Amani moyoni …

 

4.  Siogopi tena nikiitwa kufa, 

    Yu nami daima, Yesu. 

    Mlango wa mbinguni

    ni Yeye pia,

    “Tapita humo kwa damu” 

           Amani moyoni …

 

5. Nitaketi na Yeye huko milele,

   Nisifu Mwokozi wangu. 

   Nina raha moyoni majira yote

   Kwa Yesu, Mwanawe Mungu 

           Amani moyoni…


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya