434. Umechoka, Umeshushwa Moyo?

1.  Umechoka, umeshushwa moyo?

    Mwambie Yesu, mwambie Yesu;

    Una huzuni, huna furaha?

    Mwambie Yesu sasa.   

           Mwambie Yesu,  

           mwambie Yesu, 

           Amejulika sana; 

           Hayuko rafiki kama Yesu,

           Mwambie Yesu sasa.

 

2.  Unalia juu ya haja zako?

    Mwambie Yesu, mwambie Yesu;

    Mbona wazificha dhambi zako? 

    Mwambie Yesu sasa.

             Mwambie Yesu ...


3.  Waogopa? Usihuzunike,

    Mwambie Yesu, mwambie Yesu;

    Una hofu kwa mambo ya mbele?

    Mwambie Yesu sasa. 

            Mwambie Yesu...


4.  Waogopa uwazapo kifo?

    Mwambie Yesu, mwambie Yesu;

    Wautamani ufalme wake?

    Mwambie Yesu sasa. 

            Mwambie Yesu...


Popular posts from this blog

420. Ni Salama Mikononi Mwake

398. Hapana Rafiki Kama Yesu

406. Mfurahini, Haleluya